Genesis 28:13-15

13Juu yake alisimama Bwana, akasema, “Mimi ni Bwana, Mungu wa baba yako Ibrahimu na Mungu wa Isaka. Nchi ambayo umelala juu yake, nitakupa wewe na uzao wako. 14Uzao wako utakuwa kama mavumbi ya nchi, nawe utaenea upande wa magharibi na mashariki, kaskazini na kusini. Kupitia wewe na uzao wako mataifa yote ya duniani yatabarikiwa. 15Niko pamoja nawe nami nitakulinda kila uendako na nitakurudisha katika nchi hii. Sitakuacha mpaka nitakapofanya hayo niliyokuahidi.”

Copyright information for SwhKC